

Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Mhe. Abdulrahman Kinana ameendelea na ziara yake ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye maeneo mbalimbali nchini na kufanikiwa kufika Wilaya Ruangwa mkoani Lindi.
Akiwa Mgeni rasmi kwenye Mkutano mkuu CCM Wilaya ya Ruangwa, Kinana ametoa salaam za Rais Samia kwa wakazi wa Ruangwa na kuwakumbusha WanaCCM utamaduni wa chama hicho wakati wa uchaguzi kwa Rais aliyepo madarakani.
Kinana amesema >>’Chama chetu kinaongozwa na Katiba, Kanuni na Utamaduni. Utamaduni tulionao CCM, Rais anapokua kwenye awamu ya kwanza tunapenda aendelee na kwenye awamu zinazofuata, Rais Samia yuko kwenye awamu ya kwanza, kwanini asiendelee kwenye awamu ya pili? Tuna sababu? hatuna. Kama kuna wengine watajitokeza kwenye vyama vingine katiba inaruhusu lkn kwa CCM hakuna wa kutuzuia Rais Samia asiendelee’ – Kinana.
Makamu Mwenyekiti Kinana ameyasema hayo baada ya kuombwa na Wajumbe wa Mkutano Mkuu maalum wa Wilaya Ruangwa.
Mkutano huo mkuu wa Wilaya ulihudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi akiwemo Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa (Mb), Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hassan Ngoma na Viongozi wengine wa CCM.



4 Comments
Even the honeymoon period will fade away after a few years,ラブドール 値段but your marriage phase should get better every year.
Just want to say your article is as astounding. The clearness in your post is simply cool and i can assume you’re an expert on this subject. Well with your permission allow me to grab your feed to keep up to date with forthcoming post. Thanks a million and please keep up the gratifying work.
Накрутка просмотров в Телеграм канал
I blog quite often and I truly thank you for your content. Your article has truly peaked my interest. I will book mark your website and keep checking for new details about once per week. I opted in for your RSS feed too.
накрутка лайков подписчиков ётуб
This site is constantly a great place to learn new ideas and techniques. Thanks for sharing your insights with us.