Mhariri na Mtangazaji wa Channel Ten, Khamis Mkotya, ametajwa kuwa miongoni mwa wanaCCM walioonesha nia ya kugombea Ubunge katika Jimbo la Chemba mkoani Dodoma katika Uchaguzi Mkuu mwaka huu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mkotya, anayefahamika kwa jina la utani “Chemba Boy” kutokana na ukaribu wake wa muda mrefu na wananchi wa jimbo hilo, anatarajiwa kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo muda ukifika.

Hii itakuwa ni mara yake ya tatu kuwania nafasi hiyo, jambo linaloashiria dhamira yake ya dhati ya kutaka kulitumikia jimbo hilo.

Akizungumza kwa kifupi baada ya kuhojiwa juu ya tetesi hizo, Mkotya alithibitisha nia yake kwa maneno haya: “Ni kweli, nipo tayari kuchukua fomu pale muda utakapowadia kulingana na utaratibu wa chama. Chemba ni nyumbani na dhamira yangu ni kuleta mabadiliko chanya yenye tija kwa jamii yangu ya Chemba”

About Author

Bongo News

9 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *