Na Mwandishi Wetu

Mke wa Rais wa Finland, Suzanne Innes-Stubb, leo Jumanne Mei 14, 2025, amefanya “Royal Tour” kwenye Makumbusho ya Taifa Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine alifurahia sana historia ya zamadam (binadamu wa kale) na utamaduni wa Tanzania.

Akipokewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Miliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi na Mkurugenzi wa Makumbusho hiyo Dkt. Noel Luoga, Mama Suzanne Stubb, mtaalam wa sheria za Umoja wa Ulaya, ameeleza kufurahia historia ya zamadam na kueleza matamanio yake kwa watafiti kutoka nchini Finland kuja kujifunza zaidi.

About Author

Bongo News

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *