KITAIFA

RAIS SAMIA NA MGENI WAKE RAIS WA HUNGARY, MHE. KATALIN Novák, WAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI IKULU DAR ES SALAAM

RAIS SAMIA NA MGENI WAKE RAIS WA HUNGARY, MHE. KATALIN Novák, WAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI IKULU DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Hungary Mhe. Katalin Novák wakati wakizungumza na Waandishi wa Habari Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Julai, 2023. Rais Novák yupo nchini Tanzania kwa ziara ya siku tatu.

Rais wa Hungary Mhe. Katalin Novák akizungumza na Waandishi wa Habari Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Julai, 2023.

Viongozi mbalimbali pamoja na Waandishi wa Habari waliohudhuria Mkutano wa Wanahabari kuhusiana na Ziara ya Rais wa Hungary Mhe. Katalin Novák Ikulu Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na Mgeni wake Rais wa Hungary Mhe. Katalin Novák wakishuhudia Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolph Mkenda pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu kutoka
Hungary Tristan Azbej aliyeiwakilisha Wizara ya Mambo ya
Nje na Biashara ya Nchi hiyo wakati wakisaini Hati ya Makubaliano baina ya nchi mbili kuhusu Ushirikiano wa
ndani wa Programu ya Stipendium Hingaricum ya mwaka 2024-2026, Ikulu Jijini Dar es Salaam. Stipendium Hingaricum ni Programu ya ufadhili wa masomo ya Elimu ya
Juu (Scholarship) inayotolewa na Serikali ya Hungary kwa ajili ya Wanafunzi wa kigeni.

About Author

Bongo News

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *