
Novemba 2, 2023
*Asema ni kiongozi mchapakazi na mtiifu, Chama kina matumaini makubwa.

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Itikadi na Uenezi Paul Makonda amesema CCM haina shaka na utendaji kazi wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwani ni kiongozi mchapakazi na mtiifu.
“…Katika utendaji wa kazi sisi upande wa Chama tuna matumaini makubwa na uwajibikaji na uaminifu wa Waziri wetu Mkuu Kassim Majaliwa, tumemuona katika maeneo mengi akisimamia shughuli mbalimbali za Serikali na nilipotoa agizo la Chama kwa Waziri Mkuu nilitaka agizo hilo lifike kwa mtu anayeweza kuleta matokeo chanya kwa Chama.”
Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi amesema lengo la CCM chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha Serikali inatimiza kile ambacho imepewa kukifanya kwa mujibu wa ilani ya uchaguzi, hivyo wana matumaini makubwa na utendaji kazi wa Mheshimiwa Majaliwa.

Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Novemba 2, 2023) alipokwenda ofisini kwa Waziri Mkuu Bungeni jijini Dodoma. Amesema lengo la Chama ni kuhakikisha ndoto ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na kuwatumikia na kuwaletea maendeleo wananchi wote hususani wanyonge inafikiwa.
Amesema Waziri Mkuu ni mtendaji mtiifu, mwaminifu na kwamba maelezo yaliyotolewa kwake na CCM kuhusu kushughulikia migogoro ya ardhi tayari ameyapokea na ameanza kuyatekeleza. “Nina imani hata miezi sita tuliyompa inawezekana akatumia hata miezi mitatu tukapata ripoti.”
Kadhalika, Makonda amesema Chama kimemwagiza Waziri Mkuu kuwachukulia hatua wote ambao wataonekana kukwamisha utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ndani ya Serikali. “Yeyote ambaye anabainika kufanya ubadhirifu wa mali za umma na Waziri Mkuu akabaini achukue hatua mara moja na Chama tumempa baraka zote.”

Kwa upande wake, Waziri Mkuu amesema Serikali imepokea maelekezo ya Chama na kwamba itaendelea kuyafanyia kazi na kuhakikisha migogoro ya ardhi katika maeneo mbalimbali nchini inaendelea kushughulikiwa.
Akizungumzia kuhusu suala la udhibiti wa fedha za umma, Mheshimiwa Majaliwa amesema serikali itaendelea kulisimamia jukumu hilo ili fedha zinazotolewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo zitumike ipasavyo na katika viwango vya ubora vinavyotarajiwa.
7 Comments
This is incredibly beneficial; I’ve saved it for future reference.
sii2lj
¡Hi seguidores del azar
No pierdas la oportunidad de reclamar el tuyo al registrarte.
Entre las mejores casas de apuestas espaГ±olas se encuentran algunas nuevas, con interfaz moderna y sin requisitos complejos de registro.
Casas apuestas EspaГ±a con juegos exclusivos y rГЎpidos – casas de apuestas sin verificacion
¡Por muchos brillantez cómica!
?Hola jugadores
PastГіn bono 20 euros es perfecto para explorar nuevos juegos y ganar premios reales.
Juega en casinos online con 20 euros gratis y arriesga cero de tu propio dinero. – casino20eurosgratissindeposito.guru
?Que tengas excelentes ventajas!
?Hola buscadores de fortuna
Con casino 20 euros gratis sin depГіsito podrГЎs disfrutar de tragaperras, ruletas y mГЎs sin riesgos.
Apuesta en los mejores casinos de EspaГ±a y recibe 20 euros gratis sin depГіsito. – casino online regala 20 euros gratis
?Que tengas excelentes rondas de juego !
?Hola fanáticos de los juegos de azar
Marca casino 20 euros gratis ofrece bonos insuperables para quienes buscan diversiГіn gratuita.
Gana 20 euros retirables en los casinos online mГЎs seguros de EspaГ±a. – casino20eurosgratissindeposito.guru
?Que tengas excelentes sesiones de juego !
?Hola cazadores de suerte
ВїQuieres conseguir 20 euros gratis? ВЎRegГstrate y empieza a jugar con saldo real sin hacer un depГіsito!
Comienza a jugar en Playzax casino con 20 euros gratis sin realizar ningГєn ingreso. – ganar 20 euros por registrarte
?Que tengas excelentes giros afortunados !