KITAIFA

LAKE GROUP YATOA MSAADA KWA WATHIRIKA WA MAFURIKO RUFIJI

LAKE GROUP YATOA MSAADA KWA WATHIRIKA WA MAFURIKO RUFIJI

Serikali imezipongeza Kamati za Ulinzi na Usalama pamoja na Kamati za Maafa katika maeneo yote yaliyokumbwa na maafa ya mafuriko kwa namna wanavyosimamia zoezi la uokoaji na kuratibu kwa makini misaada inayotolewa kwa ajili ya waathirika.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mungano na Mazingira Dkt. Selemani Jafo ametoa pongezi hizo wilayani Rufiji, wakati aliposhuhudia Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakar Kunenge akipokea msaada wa tani 20 za chakula na Mitungi ya Gesi na Majiko yake 300 iliyotolewa na Kampuni ya Lake Energies kwa ajili ya wananchi wa wilaya ya Rufiji waliokumbwa na mafuriko.

Dkt. Jafo amesema misaada hiyo ni kielelezo cha wadau na wawekezaji nchini kuitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye yeye mwenyewe Rais amekuwa kiongozi katika kuchangia misaada hiyo kwa ajili ya watanzania wa maeneo mbalimbali yaliyokumbwa na changamoto ya mafuriko kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

About Author

Bongo News

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *