KIMATAIFA KITAIFA

SAMIA NA HAKAINDE KUONDOA VIKWAZO VYA BIASHARA TANZANIA NA ZAMBIA

SAMIA NA HAKAINDE KUONDOA VIKWAZO VYA BIASHARA TANZANIA NA ZAMBIA

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zambia, Hakainde Hichilema wameazimia kuweka mazingira yatakayofanya biashara kati ya Tanzania na Zambia zisiwe na vikwazo.

Wakizungumza katika Kongamano la Wafanyabiashara wa Tanzania na Zambia lililofanyika jana jioni marais hao walisema eneo moja la muhimu ni kuhakikisha magari hayakai kwenye mipaka kwa muda mrefu pasi na sababu.

Marais hao wanakutana kwenye mkutano wa ana kwa ana leo asubuhi na waliwaambia Wafanyabiashara hao kwamba mazungumzo yao yatajikita kwenye kuweka taratibu za kuondoa changamoto hizo.

About Author

Bongo News

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *