MICHEZO

UKAGUZI WA AFCON UMEENDA VYEMA – YAKUBU

UKAGUZI WA AFCON UMEENDA VYEMA – YAKUBU

Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw Saidi Yakubu amesema timu ya Wakaguzi kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) kwa maandalizi ya AFCON 2027 imemaliza ukaguzi wao vyema katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda kupitia kapeni ya EA Pamoja Bid.

Akiongea katika Kipindi cha Jambo kinachorushwa ya Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) Agosti 5, 2023 jijini Dar es salaam, Katibu Mkuu Bw Yakubu amesema timu hiyo imemaliza kazi yao vizuri hapa ambapo ukaguzi wao ulianzia nchini Kenya, Uganda na Tanzania na kuhitimisha kazi yao kikao cha majumuisho kilichofanyika Zanzibar.

Maeneo mengine waliyokagua ni pamoja na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, HospitaIi ya Taifa Muhimbili, Uwanja wa Amaan Zanzibar, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Hospitali ya Mnazi Moja, Uwanja wa uwanja wa Mao Tse Tung Zanzibar pamoja na hoteli zitakazotumiwa wakati wa mashindano hayo kulingana na viwango vya CAF.

“Baada ya ziara yao hiyo Kenya, Uganda na Tanzania, walifanya mkutano wa majumuisho, Hatupo vibaya, tupo vizuri. Kinachotazamwa na wakaguzi ni pamoja na utayari wa Serikali namna ilivyojipanga katika kuhakikisha tukio hili tumelipokea, ukweli ni kwamba ziara yote hii ilikuwa inaongozwa Katibu Mkuu tayari inaonesha kwamba Serikali ipo tayari” amesema Katibu Mkuu Bw Yakubu.

Vigezo zingine ambavyo wakaguzi hao wa AFCON waliangalia ni mtiririko wa matukio kuelekea AFCON, kwa maana ya miundombinu ni lazima yote ikamilike kabla ya tarehe 31 Desemba 2025, Tanzania inajenga kiwanja kipya cha Arusha ambapo walioneshwa michoro, nyaraka zote muhimu na mapango wa mtiririko wa fedha utakavyokuwa katika kukamilisha ujenzi wa uwanja huo.  

About Author

Bongo News

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *